WATOTO NI DHAHABU
Namshukuru
Muweza, Mungu mwenye huruma
Aliye
nipa kuweza, nimeamka salama
Ninaanza
na kuwaza, yale yaliyo na hekima
Watoto
kama Dhahabu, itunze itakutunza
Si
vyema kuwapuuza,watunzeni kwa adabu
Kadhalika
kuwabeza,yafaa mjitanibu
Vitendo
vya kuchukiza, msiwe navyo karibu
Watoto
kama Dhahabu, itunze itakutunza
Yafaa
kuwatuliza, bila kufanya ghadhabu
Mazuri
mkiwaeleza, watakuwa wastarabu
Hata
wakiteleza, rahisi kujinasibu
Watoto
kama Dhahabu, itunze itakutunza
Watoto
mkiwakuza, umea kama zabibu
Wakubwa
muwe wa kwanza, nyenzo zenu kuzitibu
Wadogo
wanachukiza,kuwalea kubwa tabu
Watoto
kama Dhahabu, itunze itakutunza
Wewe
Mungu kakukuza, daraja umekasibu
Na
mwana ukimtunza, atageuka dhahabu
Hatua
zake zakwaza, zinataka mahesabu
Watoto
kama Dhahabu, itunze itakutunza
Abadani
ukiweza, wewe ni bingwa tabibu
Lakini
ukiwabeza, kwa jazilizo la gubu
Utajichonga
jeneza, kujitia magadhabu
Watoto
kama Dhahabu, itunze itakutunza
Mimi
siwapi bughuza, mkafura maghadhabu
Ila
ninawaeleza, mpate japo taibu
Sifa
ya mwana kutunza, na sio kuwasulubu
Watoto
kama Dhahabu, itunze itakutunza
Mwana
anakengeza, na mwingine wa ububu
Allahu
Rabi Muweza, hugawa pasi na kubu
Hatunabudi
kutunza, pasipo ona aibu
Watoto
kama Dhahabu, itunze itakutunza
Pale
mnapo wafunza, bila kuleta aibu
Wakutoa
istiza, ukapata na swawabu
Tena
nina sisitiza, mtoto ni kama dhahabu
Watoto
kama Dhahabu, itunze itakutunza
La
mwisho la kumaliza, sikia Bwana Hatibu
Zingatia
bi Eliza, jiepushe izarabu
Usijekunishangaza,
tapokwona babu babu
Watoto
kama Dhahabu, itunze itakutunza
No comments