HILI NDIO BALAA LINGINE LA ''MKATA UMEME'' N’GOLO KANTE
Kiungo mkabaji kwa kawaida huwa ni mtu mwenye mwili uliojengeka hasa, ana fujo nyingi uwanjani na ni wachache sana wanapata tuzo kama ambavyo Mfaransa N’golo Kante anapata katika msimu wake wa pili kwenye ligi kuu nchini Uingereza.
Kante, amechaguliwa na Shirikisho la Waandishi wa Habari za Soka kuwa mchezaji bora wa mwaka wiki chache baada ya kupata tuzo nyingine ya mchezaji bora wa mwaka kutoka kwa Shirikisho la Wachezaji wa Kulipwa. Kwenye kura hizo, mchezaji mwingine wa Chelsea, Eden Hazard alishika nafasi ya pili huku Dele Alli wa Tottenham akishika nafasi ya tatu.
Congratulations to @nglkante, who has been voted the 2017 Footballer of the Year by the Football Writers' Association! 👏 pic.twitter.com/8SaWKVCkgR— Chelsea FC (@ChelseaFC) May 8, 2017
JIUNGE NASI AKISI TV KILA SIKU KUPATA HABARI ZA UHAKIKA Nini maoni yako? Weka comment yako hapa,
No comments