-->

Header Ads

MAJANGA BARCELONA, SITA HAWA MAJERUHI KUWAKOSA JUVE LEO


Timu ya FC Barcelona imekumbwa na idadi kubwa ya majeruhi kuelekea kwenye mchezo wa marudiano wa klabu bingwa barani Ulaya dhidi ya Juventus hatua ya robo fainali mchezo utakaofanyika kwenye uwanja wa Nou Camp kesho.

Wakiwa wanajiuliza watawezaje kupindua matokeo ya kichapo cha mabao 3-0 walichopata kutoka kwa Waitaliano hao wiki iliyopita miamba hiyo imepata pigo kutokana na kukumbwa na idadi kubwa ya wachezaji muhimu kupatwa na majeraha.

Wachezaji watakaokosekana kwenye mchezo huo ni Arda Turan, Gerard Pique, Sergio Busquets, Jeremy Mathieu na Javier Mascherano.

No comments

Powered by Blogger.