WITO KWENU WATUNZI
Tukutaneni
wajuzi, magwiji wa mashairi
Mafundi
na wanafunzi, Sara na bwana Bashiri
Tuje
na zetu kurunzi, tukajenge tafakari
Washairi
mwasemani, ni swala makanikia
Tutungeni
zetu tenzi, ushairi ukifana
Kama
hayati Mdanzi, mtunzi mzuri sana
Maneno
yafate ngazi, tupange yakipandana
Washairi
mwasemani, ni swala makinikia
Sisi
pia ni wahunzi, mafundi kupanga vina
Hatujadili
upuzi, uchambuzi wetu kina
Tunajulikana
wazi, ni mabingwa wa kunena
Washairi mwasemani, ni
swala makinikia
Njooni
na wakufunzi, tena nawaomba sana
Watatua
matatizi, pasipo ya kubishana
Tusiwe
na pumbuwazi, pumbazo kushangazana
Washairi mwasemani, ni swala makinikia
Tuzitumie
karama, jario la maulana
Tuitulize
mitima, tujenge hoja za maana
Tutaepuka
zahama, tukiacha chekeshana
Washairi mwasemani, ni swala makinikia
Sote
mpate raha, pendezo la subuhana
Yanini
hizi karaha, na kuzidi kushindana
Tunalifanywa
majuha, mkubwa afanywa mwana
Washairi mwasemani, ni swala makinikia
Nanyi watunzi wa nyimbo,
ninyi mnanguvu sana
Kwa ufundi wa kiimbo, na tungo
zasikikana
Tu unasue urimbo, tena
pasipo hiyana
Washairi mwasemani, ni swala makinikia

No comments