-->

Header Ads

MAJIBU YA ZITTO KABWE KUHUSU Mwenyekiti wao kuteuliwa na JPM kuwa Mkuu wa Mkoa



Moja kati ya habari zilizoshtua wengi Jumamosi ya June 3 2017 ni kuhusiana na uamuzi wa Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kumteua Mama Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Uteuzi wa Rais Magufuli umewashitua wengi kutokana na Mama Anna Elisha Mghwira kuwa ni mwenyekiti wa chama cha ACT Wazalendo na aligombea Urais wa Tanzania katika uchaguzi Mkuu 2015, hivyo wengi wanajiuliza atakubali nafasi hiyo na kama atakubali atatekeleza ilani ya chama gani CCM au ACT.

Baada ya maswali kuwa mengi kwa mmoja kati ya viongozi wa chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa jimbo la Kigoma Mjini Zitto Kabwe ameamua kutumia ukurasa wake wa facebook kuwataka watu kuwa na subira watatoa majibu.




“Nimekuwa naulizwa Sana kuhusu uteuzi wa Mwenyekiti wa Chama chetu kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro. Nimekuwa kimya Kwa sababu tumepokea Taarifa za uteuzi kutoka katika vyombo vya Habari. Mwenyekiti yuko nje ya nchi na kutokana na tofauti za masaa bado hatujawasiliana nae”

“Tutatoa tamko kamili atakapokuwa amerejea nchini. Ninawataka wanachama wote wa Act Wazalendo wawe watulivu na Kama kuna masuala yanayohusu maamuzi ya vikao vya Chama tutawajulisha. Aliyeteuliwa ni Mwenyekiti wa Chama Taifa, sio mshauri au mwanachama tu”

“Ni mmoja wa viongozi wa juu wa Chama chetu. Uteuzi wake unahitaji kikao cha Kamati Kuu ya Chama kukaa na kujadili. Nitaweza kutoa Taarifa baada ya vikao vya Kamati Kuu ya Chama. Kwa sasa umma usubiri vikao Kwa mujibu wa Katiba ya Chama chetu”

Kama utakuwa unakumbuka vizuri Mwenyekiti wa ACT Wazalendo anakuwa mtu wa tatu kutoka cha cha upinzani kuteuliwa na Rais Magufuli baada ya Augustino Mrema wa TLP  kuteuliwa kuwa mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole na Prof Kitila Mkumbo kuwa Katibu Mkuu wa wizara ya Maji na Umwagiliaji.

JIUNGE NASI AKISI TV KILA SIKU KUPATA HABARI ZA UHAKIKA Nini maoni yako? Weka comment yako hapa,

No comments

Powered by Blogger.