VYETI FEKI VILIVYOMNG'OA MUHUDUMU WA MOCHWARI..INAUMA SANA..
Sakata la vyeti fedha limemuondoa kazini mhudumu wa chumba cha
kuhifadhia maiti wa hospitali ya Mkoa wa Shinyanga baada ya kukutwa na
cheti cha kughushi.
Katibu tawala wa Shinyanga, Albert
Msovela amemtaja mtumishi huyo kuwa ni Christopher Lwambo na kusema kuwa
ndiye pekee katika hospitali hiyo aliyebainika kuwa na cheti feki.
Msovela
amesema hakuna mtumishi mwingine wa umma katika taasisi hiyo aliyenaswa
na cheti bandia na kwamba, huduma zinaendelea vizuri.
Wakati
mtumishi huyo akiondolewa, Mwenyekiti wa CCM wilayani Chamwino, Charles
Ulanga ambaye ni mratibu wa elimu wa Kata ya Buigiri ameandika barua ya
kukata rufaa lakini ametakiwa kuipeleka kwa mwajiri wake ambaye ni
mkurugenzi mtendaji wa halmashauri.
“Nilishaandika
barua, lakini tulielekezwa kuzipeleka kwa waajiri wetu ambao wao ndiyo
watazifikisha kwa wahusika. Mimi nimeshafanya hivyo,” amesema Ulanga.
Jina lake lilikuwa miongoni mwa majina yaliyojitokeza katika orodha ya watumishi wanaodaiwa kughushi vyeti.
Hata
hivyo, alijitokeza hadharani na kupinga suala hilo akisema alisoma
elimu ya msingi na baadaye ualimu bila ya kupitia elimu ya sekondari na
kuwa ndivyo vyeti alivyowasilisha.
Wakati Ulanga
akikata rufaa, Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (Talgwu)
mkoani Morogoro kimepokea wafanyakazi zaidi ya kumi wakilalamikia
kutotendewa haki.
Katibu wa Talgwu mkoani humo,
Lawrence Mdega amesema wafanyakazi hao walifika ofisini kwake
wakilalamika kuwa waliajiriwa kwa elimu ya darasa la saba, lakini
wanashangaa wameandikwa kuwa walimaliza kidato cha nne.
Mkuu
wa kitengo cha utawala na fedha wa Chuo Kikuu cha Sokoine (Sua), Yonica
Ndaga amesema watumishi watatu wa chuo hicho wameonyesha nia ya kukata
rufaa wakidai kuonewa na uhakiki uliofanyika ambao haukuwatendea haki.
JIUNGE NASI AKISI TV KILA SIKU KUPATA HABARI ZA UHAKIKA
Nini maoni yako? Weka comment yako hapa,
No comments