-->

Header Ads

ABDUL NONDO AMLIMA BARUA RC MAKONDA


BARUA YA WAZI KWA MKUU WA MKOA WA DAR. MH.PAUL MAKONDA

Habari ya majukumu mkuu wa mkoa wa Dar,mh.paul makonda natumai unaendelea vizuri na majukumu yako ya kila siku.

Mimi naitwa Abdul Omari Nondo ni mtanzania ,pia ni mkazi wa mkoa wako maeneo ya ubungo.mh.paul makonda ni leo baada ya majukumu ya wiki nzima nimepata ona kipande cha video yako youtube,ukiwa na mkutano na wafanya kazi wa mipango miji,na viongozi wengine.

Jambo ambalo limepokelewa vibaya katika jamii ni kauli ulipo onesha *kukasirishwa wafanyakazi hao walipoonesha hisia zao za kuomba mshahara uongezwe siku ya mei mosi na mabango yao mbele ya raisi* umesikika ukiwaambia kuwa hawapaswi kuongezewa na *ungekuwa wewe ndio raisi ungewachapa viboko* sababu kwamba wanasababisha migogoro ya ardhi kwa kugawa mara mbili(double allocation) haya ni maneno yako mh.mkuu wa mkoa.

Mh.paul makonda kuna theorist mmoja anaitwa Elton mayo amezungumzia juu ya motisha,hamasa kwa wafanyakazi,(motivation theory) amezungumza kuwa ili mfanya kazi afanyekazi vizuri akiwa na faraja moyoni anahitaji heshima,athaminiwe, asikilizwe,apongezwe,mshahara alipwe vizuri hapo ukitimiza haya ndio unapaswa ulalame kwa nini kazi aziendi ukiwa mahitaji yao wanapata.

Lakini wewe umeonekana kudhalilisha,ungewachapa pa bakora,kwa kuomba kuongezewa mshahara .
Mh.paul makonda,unajua maisha yako na yao kama ni tofauti saana?

Unafahamu kuwa ni hao ndio wanalipwa laki 6, au laki 7 kwa mwezi unafahamu kuwa ni hao ndio wanakatwa makato lukuki kodi(paye),bima(NHIF),mafao(NSSF/GEPF/LAPF/PSPF),vyama vya wafanyakazi(Trade union),mkopo benki(CRDB/NMB), Makato ya bodi ya mikopo(Heslb 15%).unajua kati ya laki saba au laki nane baada ya makato wanapata sh.ngapi?
Hivi unafahamu ni hawa ndio wana nunua unga sh.kl 2400,sukari 2000,gas 540000. 

Unafahamu kuwa ni hawa ndio wamepanga na kila mwezi wanalipia  kodi?? Unajua kuwa ni hao ambao watoto wao hawana mkopo chuo na wanawasomesha kwa shida?,Alafu wewe mh.paul makonda unawaambia ungewapiga bakora kwa kuomba kuongezewa mshahara. Kweli una huruma kweli,(sympath)?

Mwalim.nyerere katika kitabu cha TANU NA RAIA,ukurasa wa 6-7 ,aprili 1962  aliwahi sema
"Tulipopunguza mishahara ya Mawaziri (ambao pia ni Wabunge), tulisifiwa kwamba tumefanya jambo zuri. Na kweli tulifanya jambo zuri. Mshahara wa waziri wa kikoloni ulikuwa zaidi ya Shs.5,000 kwa mwezi, sisi tulipunguza ukawa Shs.3,000 ambao ktk sehemu nyingize za Afrika au dunia ni mshahara mdogo sana. Lakini kulinganisha mshahara wa Mawaziri wetu na mishahara ya mawaziri wa nchi nyingine, ambayo yaweza ikawa tajiri zaidi kuliko Tanganyika (Tanzania), siyo njia safi ya kulinganisha. Njia inayofaa kutumiwa, njia ambayo wana-TANU na wananchi wote hatuna budi tuitumie, ni kulinganisha mshahara huo na pato la ndugu zetu(wananchi wa kawaida). 

Basi njia safi ya kujua kama mshahara wa Sh.3,000 kwa mwezi ni mkubwa au mdogo si ile ya kuulinganisha na mishahara ambayo Mawaziri (wakiwemo na Wabunge) wa nchi nyingine hupokea. Njia bora ni kulinganisha Sh.3,000 (iliyokuwa ikipokelewa na Mawaziri) kwa mwezi na Sh.75/50 au Shs.132 kwa mwezi (iliyokuwa ikipokelewa na Watumishi wa kawaida wakati huo). Hakuna mtu anayeridhika na fedha. Kwa hiyo Mawaziri (na wabunge) wetu wanazo shida kubwa, na tunazijua. 

Lakini shida zao ni za aina mbali kabisa na shida ya mtu ambaye anapata Shs.71/50 kwa mwezi!"
Mh.paul makonda huyo ni mwalimu nyerere shida za hao wanaopokea laki 5 au laki 6 na shida zako ,au za mbunge na waziri ni shida tofauti ,lakini wewe kama hulijui hili ila unavimba na kusema ungewachapa fimbo ,
Hivi uliowaambia hivyo wanajua kuwa wewe unalipwa zaidi ya mil 4 kwa mwezi,una posho,marupurupu,gari ya serekali ,nyumba ya serekali,na una kiinua mgongo baada ya miaka 5,sh.mil 200??,wanajua hivyo ??

Je umelinganisha hiyo laki 5,au laki 6 yao wanayopokea umeona ni kubwa zaidi ya mil 4.yako?? Ndio maana unasema hawapaswi lipwa na ungewachapa fimbo??

Mh.makonda umeonesha kukasirika sababu eti unaona hawafanyi kazi kwa ufanisi,hawawezi kuwa na morale ya kazi sababu mshahara mdogo,madeni,makato,bidhaa bei ghali,na wewe unawatisha kuwachapa viboko kwa kuomba waongezewe mshahara ,mwana theory *elton mayo* anasema kwa mazingira haya usitegemee ufanisi kutoka kwa wafanyakazi. 

Ukiitaji ufanisi katika kazi lazima upande,uwekeze,uwape motisha(input) ndio utegemee ufanisi(output).sasa wewe unataka output bila input? ,what do you expect?

Umefany Makosa na kuvunja sheria ya shirika  la kazi la kimataifa(ILO) *declaration on fundamental principal and Rights at work* ya mwaka 1998.inayotaka mazingira bora ya kazi,mshahara mzuri,na inakataza harassment,chuki ,matusi ,udhalilishaji kwa wafanyakazi.

Mh.makonda elewa jamii haijapokea vizuri kauli yako kwa wafanya kazi ,elewa kiongozi bora ni anayekuwa na kauli nzuri,matendo,heshima kwa anao waongoza ndio utapata ushirikiano ,kukubalika,kupendwa,ushirikiano yaani LEGITIMACY
Naomba niishie hapa,shukrani kwa kusoma barua yangu, nakutakia majukumu mema katika utumishi wako.
Wako mtiifu.
Abdul omary Nondo
0659366125.

No comments

Powered by Blogger.