-->

Header Ads

Wateja wakosa umeme kutokana na hitilafu Kipawa

Taarifa ya Tanesco iliyotolewa leo Jumatatu Oktoba 30,2017 na ofisi ya uhusiano makao makuu imesema hitilafu imetokea saa 11:51 asubuhi.
Kutokana na hitilafu hiyo, Tanesco imesema Gongo la Mboto, Air Port, Chang'ombe na baadhi ya maeneo ya Tabata na Buguruni hayana umeme.
Shirika hilo limesema mafundi wanaendelea na jitihada za kurekebisha hitilafu hiyo na kwa haraka.
Kutokana na hilo, Tanesco imewaomba radhi wateja kwa usumbufu unaojitokeza.
Pia, limetoa tahadhari kwa wananchi kutoshika wala kukanyaga waya uliokatika au kuanguka.
 

KWA HABARI ZA HIVI PUNDE TANZANIA LEO jiunge na AKISITV na www.akisitv.com updates zote utazikuta humu

No comments

Powered by Blogger.