-->

Header Ads

KOREA KASKAZINI YAFANYA JARIBIO LINGINE LA NYUKLIA

Korea Kaskazini imefanya jaribo la sita la nyuklia kwa mujibu wa wizara ya mashauri ya nchi za kigeni ya Japan.

"Serikali inathibitisha kuwa Korea Kaskazini ilifanya jaribio la nyuklia baada ya kutathmini taarifa kuto kwa idara ya hali ya hewa na taarifa zingine, Taro Koparo aliwaambia waandishi wa habari.

Televisheni ya taifa ya Korea Kaskazini inasema kuwa itatoa tangazo kuu muda mfupi unaokuja.

Mzozo wa Korea Kaskazini na Marekani kwa muktasariChina 'yaeleza wasiwasi' kuhusu Korea KaskaziniMarekani: Hatutaivumilia tena Korea Kaskazini

Watabiri wa hali ya hewa mapema walitambua tetemeo dogo la ardhi, eneo ambapo Korea Kaskazini ilikuwa imefanyia majaribio ya nyuklia awali.

Tetemeko hilo dogo lilitokea saa kadha baada ya kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un kupiwa picha akiwa na kile ambacho vyombo vya habari vilisema kwa liliku ni aina mpya ya bomu la hydrogen.

Vyombo vya habari vilisema kuwa kifaa hicho kinaweza kutundikwa kwenye kombora la masafa marefu.

Korea Kaskazini ilisema kuwa tetemeo hilo la ardhi lilitokea katika kaunti ya Kilju, lilipo eneo la kufanyia majaribio ya nyuklia la Punggye-ri.

China yataka Marekani na Korea Kaskazini kuvumilianaWamarekani kupigwa 'marufuku kuzuru Korea Kaskazini''Kifaa' cha Korea Kaskazini chashambuliwa na K. Kusini

Muda baadaye Rais wa Korea Kaskazini Moon Jae-in aliita mkutanao wa dharura wa baraza za lake la usalama wa taifa.

Ripoti za awali kutoka kwa idara ya hali ya hewa ya Marekani zilitaja tetemeko hilo kuw la ukubwa kwa 5.6 lakini baadaye likasema kuwa ukubwa huo ni wa 6.3 katika vipimo vya richa. HII H



No comments

Powered by Blogger.