-->

Header Ads

SIMULIZI MPYA YA KUSISIMUA IITWAYO ''UKURASA MPYA'' SEHEMU YA KWANZA HII HAPA

SEHEMU YA KWANZA



''..Si kitu rahisi sana kwa mtu kama mimi Daniel, tena mwandishi maarufu niliye bobea na kutambulika na watu wengi sana hapa nchini na hadi nje..!''
Haya yalikuwa maneno ya Daniel ambayo alikuwa anajisemea kila kona aliyopita,
Watu wengi walipenda kumsalimia kila apitapo lakini hakuwa anawaitikia ingawa hali hiyo haikuwa kawaida yake kabisa.
Watu wengine walisema labda kuna kitu anawaza au kuna jambo lina mchagiza ingawa wengine pia walikuwa wanaimani huenda kuna kitu kikubwa anaandaa, hivyo walijipa moyo na kukaa mkao wa kula kusubiri ujio mpya wa Daniel.
Moja ya mdau wake mkubwa aliyetambulika kwa jina la Baraka alijisemea, ‘‘sisi ni wadau wake wa nguvu sana hawezi kutukaushia kama hivi kwakuwa hata yeye anatambua jinsi gani tunavyopenda kazi zake kwahiyo bado najipa moyo kuwa anaandaa kitu kabambe kwani huwa hakosei asee..’’
Daniel alionekana kuchanganyikiwa na kitu maana hakuwa na furaha kabisa na alirudi mapema sana toka kazini ambavyo sio kawaida yake kabisa.
Kila mtu aliyekutana naye alitamani kujua nini hasa kinamsibu mwandishi huyo mwenye jina kubwa nchini.
Daniel alikuwa akiishi kwenye nyumba kubwa ya kifahari aliyopewa na kampuni aliyokuwa akifanyia kazi na siku hiyo alienda moja kwa moja hadi kwenye jumbna hilo hasiweze hata kuongea neno na watu aliokutana nao njiani. 
Mbali na juhudi zake za kazi amabazo zinamfanya kuingiza kipato kizuri, Daniel alikuwa kijana mtanashati,mcheshi na mkarimu sana, mara nyingi alipenda sana kuweasaidia watu wenye kuhitaji,na mda mwngine akiwa nje ya kazi hupenda sana kutaniana na wadau wake ama rafiki na ndugu wanaomzunguka.
Lakini ilikuwa tofauti sana kwa siku hiyo ambapo Daniel alipoingia ndani kwake kwenye hilo jumba la kifahari hakutoka tena.
Ni jambo lililowashangaza wengi sana hata wale jirani zake  na hata kuwapelekea kupata shauku ya kutaka kujua nini kimemkuta Daniel siku hiyo na ikawa hivyo mpaka jua lilipo chwea hakuweza kuonekana tena.

INAENDELEA...........




TOA MAONI YAKO.






No comments

Powered by Blogger.