-->

Header Ads

Uholanzi yafunga bomba lake la mafuta Nigeria kwa hofu ya uharibifu wa waasi

Shirila la mafuta la Uholanzi na Uingereza la Royal Dutch Shell, limefunga bomba muhimu la mafuta kusini mwa Nigeria kutokana na ongezeko la vitendo vya uharibifu vinavyofanywa na makundi ya waasi eneo hilo.
Taarifa iliyotolewa na nchini Nigeria ambalo ni tawi la shirika kubwa la  Royal Dutch Shell barani Afrika limetangaza kuwa, kutokana na sababu za hujuma za waasi kukiwemo kuripuliwa bomba hilo la kusafirishia mafuta, limeamua kufunga bomba hilo kwa sasa.
Shirika la mafutala Royal Dutch Shell
Makundi ya waasi kama vile kundi la wanamgambo linalojiita Walipizaji Kisasi wa Niger Delta la kusini mwa nchi hiyo  ambalo linaitaka serikali kugawa utajiri unaotokana na mafuta kwa uadilifu limekuwa likihusika na mashambulizi kadhaa dhidi ya mabomba ya kusafirishia mafuta katika maeneo tofauti ya Nigeria. Kuzorota usalama katika maeneo tofauti ya nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika, kumeyafanya baadhi ya mashirika ya mafuta kusimamisha shughuli zao nchini humo. Mwaka 1993 shirila la mafuta la Royal Dutch Shell, lililazimika kusimamisha shughuli za uzalishaji mafuta katika moja ya maeneo ya kusini mwa Nigeria.
Wanamgambo wa undi la waasi wa Niger Delta la kusini mwa nchi hiyo 
Katika hatua nyingine watu 20 wameripotiwa kuuawa na kujeruhiwa katika mashambulizi ya kigaidi yaliyofanywa na magaidi wawili wa kiume na kike katika kambi ya wakimbizi karibu na mji wa kaskazini wa Maiduguri nchini humo. Habari zaidi zinasema kuwa, katika hujuma hiyo watu watatu wameuawa na wengine 17 kujeruhiwa. Hii ni katika hali ambayo Jumatatu iliyopita pia watu wanane waliuawa na wengine 15 kujeruhiwa katika miripuko ya mabomu iliyofanywa na wanawake kadhaa katika kambi hiyo ya wakimbizi.




JIUNGE NASI AKISI TV KILA SIKU KUPATA HABARI ZA UHAKIKA Nini maoni yako? Weka comment yako hapa,
Powered by Blogger.