MH.SAMIA SULUHU HASSAN AWATAJA WANAWAKE WENYE MAFANIKIO MAKUBWA NCHINI
Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, amewataja Bibi Titi Mohammed, Thabita Siwale,
Getrude Mongela, Amina Salum Ally na Dakt. Asha-Rose Migiro kuwa ni wanawake
wenye mafanikio makubwa kuanzia ngazi za familia, Taifa hadi Kimataifa tangu
kipindi cha baada ya uhuru.
Mh. Suluhu aliyasema hayo leo kwenye hafla ya
kukabidhiwa fimbo ya kuwa mlezi wa Tanzania Girl Guides Association(TGGA)
iliyofanyika Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam.
Aidha Mh. Suluhu amemuunga mkono Mama Salma Kikwete, mke wa rais mstaafu wa awamu ya nne, Dakt. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa wanawake wanatakiwa kuchagua watu wenye mafanikio na kuwafanya kama mfano wa kuigwa.
Aidha Mh. Suluhu amemuunga mkono Mama Salma Kikwete, mke wa rais mstaafu wa awamu ya nne, Dakt. Jakaya Mrisho Kikwete kuwa wanawake wanatakiwa kuchagua watu wenye mafanikio na kuwafanya kama mfano wa kuigwa.
‘‘Kwa jinsi ninavyowaona mliopa hapa leo sina shaka
kabisa kwamba uwezo huo mnao kama ilivyo kwa wenzenu mnao wawakilisha leo hapa
na kama Mheshimiwa Mama Salma Kikwete alivyosema katika hotuba yake kwamba muwe
tayari kuchagua wanawake wenye mafanikio ili wawe ‘role models’ wenu katika
kuzifikia ndoto za kuwa na maisha mazuri’ alisema Mh.Samia Suluhu.
Pia alisistiza na kuwatia moyo wanawake wote waliojiunga na chama hiko kuwa endapo watayafata na kuyaishi kwa vitendo mafunzo yanayotolewa ndani ya chama hiko watafikia hatua kubwa walizofika wanawake hao.
Pia alisistiza na kuwatia moyo wanawake wote waliojiunga na chama hiko kuwa endapo watayafata na kuyaishi kwa vitendo mafunzo yanayotolewa ndani ya chama hiko watafikia hatua kubwa walizofika wanawake hao.
Katika hafla hiyo Mh.Mama Salma Kikwete alikabidhi
kifimbo cha malezi ya chama hicho(TGGA) kwa Makamu wa Rais baada ya yeye kuwa
mlezi kwa kipindi cha miaka 12.
Hatimaye Mh. Samia Suluhu aliwasihi wananchi kuiunga mkono Serikali kwa juhudi zinazoendelea kufanyika katika kuhakikisha Taifa linajengeka kwa misingi ya uadilifu.
Hatimaye Mh. Samia Suluhu aliwasihi wananchi kuiunga mkono Serikali kwa juhudi zinazoendelea kufanyika katika kuhakikisha Taifa linajengeka kwa misingi ya uadilifu.
‘‘Hivyo ninawasihi wananchi kuiunga mkono Serikali
hasa pale tunapochukua hatua dhidi ya wahusika wa vitendo vinavyokiuka maadili
yetu ya kitanzania ukiwamo uadilifu’’Alisisitiza Makamu wa Rais .

No comments