-->

Header Ads

MANENO YA SPIKA WA BUNGE BAADA YA KIFO CHA MBUNGE WA ZAMANI WA MOSHI MJINI NDESAMBURO


Spika wa Bunge, Job Ndugai amesema anamkumbuka marehemu Phillemon Ndesamburo kwa uchapakazi wake na mapenzi yake makubwa kwa wapiga kura wake.

“Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha Mheshimiwa Ndesamburo ambaye pia ni baba wa Mbunge wa Viti Maalum,  Lucy Owenya kilichotokea leo Mkoani Kilimanjaro, hakika ni pigo kubwa,”amesema Spika katika taarifa iliyotumwa leo  na Kitengo cha Mawasiliano cha ofisi yake

Ndesamburo amefariki leo wakati akipata matibabu katika hospitali ya Rufaa ya KCMC.

Taarifa hiyo imeongeza; "Namkumbuka vyema marehemu Ndesamburo na tuliingia Bungeni pamoja mwaka 2000, alikuwa na mapenzi makubwa kwa wapiga Kura wake."


JIUNGE NASI AKISI TV KILA SIKU KUPATA HABARI ZA UHAKIKA Nini maoni yako? Weka comment yako hapa,

No comments

Powered by Blogger.