-->

Header Ads

TAHARUKI: AFRIKA KUSINI YAHOFIWA KUWA NCHI YA KIMAFIA..WANANCHI WACHARUKA..


Sambamba na kuendelea mivutano na malalamiko nchini Afrika Kusini, Makamu wa Rais wa nchi hiyo ametahadharisha kuhusiana na hatari ya kubadilika nchi hiyo kuwa ya Kimafia.

Cyril Ramaphosa Makamu wa Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini sanjari na  kumkosoa rais huyo amesisitiza kuwa, kama chama tawala wa ANC kinataka kisipoteze himaya na udhibiti wa jamii ya nchi hiyo, basi hakipaswi kuruhusu Afrika Kusini igeuke na kuwa nchi ya kimafia. Ramaphosa ametoa wito wa kuweko uchunguzi huru kuhusiana na mafaili ya ufisadi ambayo yanawatilia alama ya swali baadhi ya viongozi wa ngazi za juu wa nchi hiyo.

Cyril Ramaphosa ametoa matamshi hayo katika hali ambayo, chama tawala cha  ANC Disemba mwaka huu kinatarajiwa kumtangaza mrithi wa Rais Jacob Zuma ambaye atapeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao uliopangwa kufanyika mwaka 2019. Ramaphosa anatajwa kuwa mgombea mkuu katika kinyang'anyiro cha uchaguzi wa chama wa kumteua mgombea wake.


Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini

Kwa muda sasa utendaji wa Rais Jacob Zuma umekuwa ukiandamwa na wimbi la ukosoaji wa vyama mbalimbali vya upinzani vya nchi hiyo. Tangu Rais Zuma alipoingia madarakani mwaka 2009 amekuwa akikabiliwa na mafaili mbalimbali ya ufisadi wa kifedha. Hata kama daima Rais Zuma amekuwa ni mwenye kukana tuhuma dhidi yake na wakati mwingine hata kuahidi kuwachukulia hatua wahalifu katika uwanja huo, lakini wanaharakati wa masuala ya kisiasa nchini Afrika Kusini na akthari ya vyama vya kisiasa vya nchi hiyo vimekuwa vikimtaka kiongozi huyo ajiuzulu na kuachia ngazi kabla ya kumalizika kipindi chake cha uongozi.

Baada ya hivi karibuni kushika kasi malalamiko, Rais Zuma akiwa na lengo la kupunguza joto la upinzani huo alimfuta kazi Waziri wa Fedha Pravin Gordhan. Hata hivyo kinyume na matarajio yake, hatua hiyo ilichochea zaidi moto wa upinzani dhidi yake. Rais wa Afrika Kusini alitaja sababu ya kumfuta kazi waziri huyo kwamba, ni katika juhudi za kupambana na ufisadi. Hata hivyo wapinzani wanapinga hilo na kusisitiza kwamba, Pravin Gordhan alifutwa kazi kwa sababu za kisiasa kutokana na waziri huyo kufichua upokeaji rushwa wa Rais Zuma.

JIUNGE NASI AKISI TV KILA SIKU KUPATA HABARI ZA UHAKIKA Nini maoni yako? Weka comment yako hapa,

No comments

Powered by Blogger.