-->

Header Ads

MATOKEO YA MICHEZO YA LIGI KUU VODACOM LEO JUMAMOSI 7 MAY 2017

AKISI TV inakuletea matokeo ya mechi zilizochezwa siku ya leo Jumamosi


Michezo Ligi Kuu Tanzania Bara iliendelea siku ya jana Jumamosi, kwa mechi tano kupigwa kwenye viwanja tofauti tofauti

Kama ilivyo ada, Goal inakuletea matokeo ya mechi zilizo chezwa siku ya Jumamosi

Yanga 2-0 Tanzania Prisons


Klabu ya Yanga imefanikiwa kukamata usukani kwa kufikisha pointing 59 baada ya kuibuka na ushindi wa goli mbili kwa bila dhidi ya Prisons

Magoli ya kipindi cha pili ya Mrundi Tambwe na Chirwa yametosha kuipa Yanga alama tatu muhimu huku Prisons wakibaki na alama zao 31 tofauti ya pointi 4 kwenye nafasi ya kushuka daraja


Majimaji 3-0 Mwadui


Majimaji ya Songea wamefufua matumaini ya kubakia Ligi Kuu msimu ujao baada ya ushindi mnono ya goli tatu kwa bila, magoli ya Kelvin Sabato, Peter Mapunda na Iddy Chipwagile

Kwa ushindi huo kumeifanya Majimaji kufikisha alama 29 kwenye msimamo


Toto African 2-1 JKT Ruvu


Rasmi klabu ya JKT Ruvu imekuwa timu ya kwanza kushuka daraja baada ya kukubali kipigo cha goli mbili kwa moja dhidi ya TOT0, magoli mawili ya mshambuliaji Wazir Junior yalitosha kuipa ushindi TOTO na kufufua matumaini kwa klabu hiyo ya kuepuka kushuka daraja

Azam 3-1 Mbao FC


Klabu ya Mbao Fc ya jijini Mwanza imejiweka kwenye mazingira magumu ya kushuka daraja baada ya kupokea kipigo cha goli tatu kwa moja na Azam
Waoka mikate wa Azam wameendelea kukamatia nafasi ya licha ya ushindi huo mzuri wa magoli matatu kwa moja, shukrani kwa washambuliaji Shabani Iddi aliyefunga mawili na John Bocco

JIUNGE NASI AKISI TV KILA SIKU KUPATA HABARI ZA UHAKIKA Nini maoni yako? Weka comment yako hapa,

No comments

Powered by Blogger.