-->

Header Ads

JEURI SASA DIAMOND PLATINUMZ Awachana Clouds Fm na EFM,Adai Hategemei Kiki Kutoka Kwao Ili Afanikiwe..!!


Diamond Platnumz amesema kwa sasa redio na TV si vyombo anavyovitegemea sana kwaajili ya promotion pindi anapokuwa akiachia nyimbo.

“Mimi nikiwa natoa nyimbo yangu, promotion yangu siwazi redio wala siwazi TV, ever. Promotion yangu ya kwanza mimi nawaza nyimbo iwafikiaje watu, kuna mitandao ya kijamii, kuna digital platform nyingi,” staa huyo alisema kwenye kipindi cha Ngaz Kwa Ngaz.

Alidai kuwa zama za kundi Fulani la watu likiamua kumrudisha nyuma msanii, halipo tena kwa wasanii wenye nguvu kama yeye.

“Tufute zile ‘naweza nikamdhuru mtu fulani ninavyotaka mimi’ vile vitu havipo tena,” aliongeza.

No comments

Powered by Blogger.