-->

Header Ads

AGNES MASOGANGE ATIWA MBARONI KWA TUHUMA ZA KUJIHUSISHA NA DAWA ZA KULEVYA

Agnes Masogange

TAARIFA zilizotufikia, zinaeleza kwamba video queen maarufuBongo, anayefahamika kutokana na shepu yake matata, Agness Gerald almaarufu Masogange, anashikiliwa na Jeshi la Polisi, Kituo Kikuu (Central) akituhumiwa kuhusika na biashara na matumizi ya madawa ya kulevya.

Masogange alikamatwa na polisi juzi usiku na taarifa zinaeleza kwamba, mpaka muda huu bado anashikiliwa central. Mwanadada huyo anaingia kwenye orodha ya wasanii wengine na watu maarufu Bongo, walioshikiliwa na wanaoendelea kushikiliwa wakihusishhwa na ishu ya matumizi na biashara ya madawa ya kulevya, katika vita kali inayoongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda

No comments

Powered by Blogger.