-->

Header Ads

Dunia yalaani hatua ya Trump kuwazuia Waislamu kuingia Marekani


Hatua ya rais Donald Trump kuwazuia wahamiaji Waislamu kuingia nchini humo inaendelea kulaani na kukoslewa kote duniani na Marekani kwenywe.

Taasisi mbali mbali za kimataifa zimeitaja hatua hiyo ya Trump ya kuwazui Waislamu kutoka baadhi ya nchi kuingia Marekani ni ubaguzi wa rangi na dhidi ya ubinadmau.

Katika taarifa, Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR na Shirika la Kimataifa la Uhamiaji IOM yametoa taarifa yakitaka Marekani iendelee kuwapokea wakimbizi na wahajiri. Pia Mashirika hayo yamesema yanaamini kuwa wakimbizi wanastahili kutendewa usawa katika kupata ulinzi, msaada na fursa za kupewa makazi bila kujali dini, utaifa au rangi.

Nchi za Iraq, Yemen na Somalia ambazo raia wake wameathiriwa na hatua hiyo zimetoa taarifa na kulaani uamuzi wa kuwazui raia wao Waislamu kuingia Marekani. Harakati ya Ansarullah ya Yemen imelaani hatua ya Marekani kuwataja raia wao nchi hiyo kuwa eti ni magaidi.

Wabunge nchini Iraq pia wamelaani hatua hiyo ya Marekani na kusema watachunguza upya uhusiano wao na Marekani katika vita dhidi ya kundi la kigaidi la ISIS.


No comments

Powered by Blogger.