-->

Header Ads

Waziri wa mifugo na Uvuvi amepiga marufuku Uuzwaji Holela wa wanyama Wanaokamatwa Kwenye Hifadhi

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mh.Luhaga Mpina amemepiga marufuku mifugo inayokamatwa kwenye hifadhi mbalimbali nchini kupigwa mnada bila maafisa mifugo kuipima na kujiridhisha ili kuepuka kuenea kwa magonjwa ya wanyama hao sambamba na kuwachukulia hatua kali wananchi ambao wamekuwa wakipokea na kubeba dhamana ya mifugo kutoka nje ya nchi huku wakidai kuwa ni ya kwao.
Akishiriki zoezi la ukamataji wa mifugo zaidi ya mia moja na sabini iliyoingia wilayani Kasulu mkoani Kigoma kutoka nchi jirani ya Rwanda Waziri Mpina amesema ni kinyume cha sheria na amewataka wafugaji wanaokamatiwa mifugo yao kujitokeza mara moja ili kuepuka usumbufu unaojitokeza.
Aidha Waziri Mpina amesema serikali itaendelea kuwachukulia hatua kali wananchi ambao wamekuwa wakipokea na kukubali kubeba dhamana ya mifugo kutoka nje ya nchi huku wakidai kuwa ni ya kwao.




KWA HABARI ZA HIVI PUNDE TANZANIA LEO jiunge na AKISITV na www.akisitv.com updates zote utazikuta humu

No comments

Powered by Blogger.