-->

Header Ads

Polisi 130 wa Afghanistan wajisalimisha kwa magaidi wa Taleban


Kwa akali polisi 130 wa serikali ya Afghanistan wamejisalimisha kwa wanachama wa kundi la kigaidi na Kiwahabi la Taleban kufuatia kudhibitiwa mji wa Kohestan mkoa wa Faryab, kaskazini mwa Afghanistan.
Abdul-Karim Yuresh, msemaji wa polisi wa mkoa wa  Faryab sambamba na kuthibitisha habari hiyo amesema kuwa, polisi wengine 200 bado wanazingirwa na wapiganaji wa kundi hilo la Kiwahabi katika eneo la Ghaleh Kheyr Abad la mji wa Kohestan. Taarifa iliyotolewa na kundi la Taleban imesema kuwa, linaendeleza mwenendo wake wa kuwafanya askari wote wa nchi hiyo wajisalimishe kwake.
Wanachama wa kundi la kigaidi la Taleban
Siku mbili zilizopita, kundi la hilo lilishambulia miji ya Bilchiragh na Dolatabad katika mkoa wa Faryab, kaskazini mwa nchi hiyo ambapo katika hujuma hiyo lilidhibiti vijiji na vituo saba vya polisi. Kadhalika kundi hilo lilishadidisha mashambulizi ndani ya wiki iliyopita kuvilenga vituo vya polisi vya wilaya ya Qaysar katika mkoa wa Faryab na kuua polisi kadhaa. Hii ni katika hali ambayo hadi sasa vyombo vya habari vimeripoti kuendelea mapigano makali kati ya askari wa serikali na wapiganaji wa kundi hilo. Makundi ya kigaidi yenye kufuata idolojia ya Uwahabi, hususan Taleban, al-Qaidah na Daesh yanaendesha harakati zao nchini Afghanistan, licha ya uepo wa vikosi vya jeshi kutoka nchi za Magharibi zikiongozwa na Marekani.
Askari wa MArekani wakiwa nchini humo
Marekani na washirika wake waliishambulia Afghanistan mwaka 2001 kwa madai ya kukabiliana na ugaidi, katika hali ambayo uepo wa askari hao wa kigeni nchini humo, ndio umechangia ongezeko la ugaidi huo.  


JIUNGE NASI AKISI TV KILA SIKU KUPATA HABARI ZA UHAKIKA Nini maoni yako? Weka comment yako hapa,

No comments

Powered by Blogger.