KIBITI JASHO LA DAMU
Sisi
wana Tanzania, Baba na akina mama
Kwanini
twajililia, twatakiwa kusimama
Wao
wanafikiria, hadha haiachi koma
Kibiti
ni fumbo gani,Amiri ulitatuwe
Tusiwe
mapunguani, tusiojua alama
Inayotakiwa
kani, kuulilia uzima
Kupigana
mapigani, wima hata kuchutama
Kibiti
ni fumbo gani,Amiri ulitatuwe
Hili
jambo si utani, legelege kusimama
Si
utani wa jirani,na mzaliwa na mama
Tulinde
yetu amani, watu tukae salama
Kibiti
ni fumbo gani,Amiri ulitatuwe
Tuipeleke
amani,kwa akili na hekima
Busara
ziwe vichwani,tupambane tukipima
Jambo
si la vitabuni,tulitafakari vema
Kibiti
ni fumbo gani,Amiri ulitatuwe
Wana
hawatoki ndani,Wawahofia khasima
Kama
tulivyo amini,tangu zamani za zama
Hii
nchi ya amani , yafatani i dhahama
Kibiti
ni fumbo gani,Amiri ulitatuwe
Mzandiki
mhaini, wala hana nia njema
Hatutaki
watudhani, jinga lenye kukoroma
Jinga
la moto jikoni, likizimwa hufuruma
Kibiti
ni fumbo gani,Amiri ulitatuwe
Huu
wetu mtihani, haraka kuusukuma
Haijai
kiganjani, sehemu yenye unyama
Tunakesha
maofisini, bila hata kusimama
Kibiti
ni fumbo gani,Amiri ulitatuwe
Amiri
msikiani, na hili ulisikize
Kibiti
ni mtihani, haraka ukatatuze
Wale
wana watanzani, wataka uwaliwaze
Kibiti
ni fumbo gani,Amiri ulitatuwe
No comments