-->

Header Ads

Winnie Mandela alazwa hospitalini Johannesburg.


Shujaa aliyepinga ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini Winnie Madikizela-Mandela, amelazwa hospitalii kwa kile kinachotajwa kuwa kufanyiwa uchunguzi wa kiafya.

Familia yake inasema kuwa alipelekwa hospitali ya Milpark mjini Johannesburg.

Mwezi Disemba mwaka uliopita, Bi Madikizela-Mandela alilazwa hospitali hiyo lakini kile kilichosababisha alazwe hakikutajwa.

Msemaji wake Victor Dlamini, aliambia BBC kuwa alikuwa ameenda kufanyiwa uchunguzi wa kawaida lakini madaktari wakaamua kumlaza.

Bi Madikizela-Mandela alikuwa mke wa Nelson Mandela, na alikuwa mwanamke wa kwanza mweusi kusajiliwa kama mhudumu wa kijamii nchini Afrika Kusini.

No comments

Powered by Blogger.